Njia ya kupanga uzazi kwa kutumia Kalenda/ Kuzuia Mimba Kwa Njia ya Kalenda
Hii ni njia ambayo mwanamke anaweza kutumia kupanga uzazi bila kutumia
dawa au kitu cha aina yoyote. Njia hii inategemea kuchagua kwa makini siku za
kufanya mapenzi kutegemeana na ufahamu wa kipindi chote cha hedhi cha
mwanamke.
Njia hii ina faida yake, lakini yeyote anayeitumia lazima awe makini sana, kwa sababu lazima ajue lini anategemea kupata damu ya hedhi tena. Ni rahisi sana kufanya makosa kwa kutumia njia hii, kwa hiyo pamoja na kutoa maelezo ya jinsi ya kutumia, sisi hatumshauri mtu kutumia njia hiyo. dawa au kitu cha aina yoyote. Njia hii inategemea kuchagua kwa makini siku za
kufanya mapenzi kutegemeana na ufahamu wa kipindi chote cha hedhi cha
mwanamke.
Nani anaweza kutumia njia ya kalenda
Moja, Wanawake walioko tayari kuchukua miezi 3 hadi 6 kupima vipindi vyao vya hedhi kabla ya kutumia njia hiyo.
Pili, Wanawake walio na mzunguko wa hedhi ambayo urefu wake
haubadiliki.
haubadiliki.
Tatu, Wanawake wanaojua hisabati vizuri sana.
Kwa hiyo, kabla ya kutumia njia hiyo, ni vyema kwa mwanamke
kuandaa kalenda
kuandaa kalenda
inayoonesha siku yake ya kwanza kutoa damu ya hedhi kila mwezi
kwa
kipindi
kwa
kipindi
cha miezi 3 hadi 6. Hii itamsaidia kujua lini mayai yake yalipevuka.
Njia hii
Njia hii
inamsaidia zaidi mwanamke aliye na mzunguko wa hedhi wa siku 28, na
hutegemea kufahamu kuwa yai la mwanamke hupevuka siku 14 kabla hajaingina
kwenye hedhi.
Kwa mfano;
1. Kama unaanza kuingia katika hedhi tarehe 1 Juni (na una mzunguko wa hedhi
wa siku 28), basi kuna uwezekano mkubwa utaingia kwenye kipindi kipya cha
hedhi tarehe 29 Juni. Kwa hiyo yai lako litapevuka siku 14 kabla kwenye tarehe 15
Juni. Kwa hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa kwako wewe kupata mimba kama
unafanya mapenzi karibu na tarehe hii, kuanzia tarehe 14 Juni hadi 16 Juni.
Kwa
hiyo kuepukana na kupata mimba, usifanye mapenzi kati ya tarehe hizo. Lakini
lazima ukumbuke kuwa mbegu za kiume zinaweza kuishi ndani ya mwili wa
mwanamke kwa siku 7, kwa hiyo ili kuwa na uhakika Zaidi ya kuepukana na
kupata mimba, una takiwa kutokufanya mapenzi kuanzia tarehe 8 hadi 16 Juni.
2. Katika mfano mwingine, kama unaanza kuingia katika hedhi tarehe 13 Juni (na
una mzunguko wa hedhi wa siku 28), basi kuna uwezekano mkubwa utaingia
kwenye kipindi kipya cha hedhi tarehe 11 Julai. Kwa hiyo yai lako litapevuka siku
14 kabla kwenye tarehe 28 Juni. Kwa hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa kwako
wewe kupata mimba kama unafanya mapenzi kati ya tarehe 27 Juni na 29 Juni.
Ili kuepukana na kupata mimba, usifanye mapenzi kati ya tarehe hizo. Kwa
usalama zaidi, usifanye mapenzi kuanzia 21 hadi 29 Juni.
kwenye kipindi kipya cha hedhi tarehe 11 Julai. Kwa hiyo yai lako litapevuka siku
14 kabla kwenye tarehe 28 Juni. Kwa hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa kwako
wewe kupata mimba kama unafanya mapenzi kati ya tarehe 27 Juni na 29 Juni.
Ili kuepukana na kupata mimba, usifanye mapenzi kati ya tarehe hizo. Kwa
usalama zaidi, usifanye mapenzi kuanzia 21 hadi 29 Juni.
3. Katika mfano mwingine, kama baada ya kuandaa kalenda kuonesha mzunguko
wako wa hedhi wa miezi 3 hadi 6 iliyopita, unagundua kuwa mzunguko wako ni
wa siku 33 badala ya siku 28, basi kifuatacho ni kweli: kama unaanza kuingia
katika hedhi tarehe 1 Juni basi kuna uwezekano mkubwa utaingia kwenye kipindi
kipya cha hedhi tarehe 4 Julai. Kwa hiyo yai lako litapevuka kwenye tarehe 20
Juni (Siku 14 kabla ya tarehe 4 Julai). Kwa hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa
kwako wewe kupata mimba kama unafanya mapenzi kati ya tarehe 19 na 21 Juni.
Ili kuepukana na kupata mimba, usifanye mapenzi kati ya tarehe hizo. Kwa
usalama zaidi, usifanye mapenzi kuanzia 13 hadi 21 Juni.
wako wa hedhi wa miezi 3 hadi 6 iliyopita, unagundua kuwa mzunguko wako ni
wa siku 33 badala ya siku 28, basi kifuatacho ni kweli: kama unaanza kuingia
katika hedhi tarehe 1 Juni basi kuna uwezekano mkubwa utaingia kwenye kipindi
kipya cha hedhi tarehe 4 Julai. Kwa hiyo yai lako litapevuka kwenye tarehe 20
Juni (Siku 14 kabla ya tarehe 4 Julai). Kwa hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa
kwako wewe kupata mimba kama unafanya mapenzi kati ya tarehe 19 na 21 Juni.
Ili kuepukana na kupata mimba, usifanye mapenzi kati ya tarehe hizo. Kwa
usalama zaidi, usifanye mapenzi kuanzia 13 hadi 21 Juni.
4. Katika mfano mwingine, kama baada ya kuandaa kalenda kuonesha mzunguko
wako wa hedhi wa miezi 3 hadi 6 iliyopita, unagundua kuwa mzunguko wako ni
wa siku 26 badala ya siku 28, basi kifuatacho ni kweli: kama unaanza kuingia
katika hedhi tarehe 1 Juni basi kuna uwezekano mkubwa utaingia kwenye kipindi
kipya cha hedhi tarehe 27 Juni. Kwa hiyo yai lako kitapevuka kwenye tarehe 13
Juni (Siku 14 kabla ya tarehe 27 Juni). Kwa hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa
kwako wewe kupata mimba kama unafanya mapenzi kati ya tarehe 12 na 14 Juni.
Ili kuepukana na kupata mimba, usifanye mapenzi kati ya tarehe hizo. Kwa
usalama zaidi, usifanye mapenzi kuanzia 6 hadi 14 Juni.
Faida ya kutumia njia hiyo
MOJA, Haina madhara yeyote ya kimwili.
Matatizo yanayoweza kujitokeza
MOJA, Njia ya kalenda si kinga dhidi ya virusi vya UKIMWI na magonjwa
mengine ya zinaa.
PILI, Njia hii ni ngumu na inahitaji wanawake kuwa wastadi katika hisabati, na
kuwa waangalifu sana kuandika au kukumbuka tarehe ya kuanza kipindi chao
cha hedhi cha mwisho.
TATU, Huchukua muda mrefu (miezi 3 hadi 6) kufahamu urefu wa mzunguko
cha hedhi.
TATU, Mzunguko wa hedhi huweza kubadilika wakati wowote kufuatana na
mabadiliko katika mwili. Hii huweza kusababisha tarehe ya yai kupevuka kuwahi
au kuchelewa, kwa hiyo mwanamke huweza kujiweka katika hatari ya kupata
mimba bila kufahamu.
NNE, Ili njia hii iwe na uhakika, mwanamke hawezi kufanya mapenzi katika siku
zake 9 kila mwezi ambapo kuna uwezekano wa yeye kupata mimba. Kwa hiyo njia
hii inahitaji uwezo mkubwa wa kujidhibiti na hufanya kazi vizuri iwapo
mwanaume namwanamke wamekubaliana kufanya hivyo kwa pamoja, na
mwanaume anamsaidia mwanamke kuhesabu au kuandika urefu wa mzunguko
wake wa hedhi.
TANO, Kwa sababu urefu wa mzunguko wa hedhi wa mwanamke huweza
kubadilika ghafla bila kutegemea, hata kama inatumika inavyotakiwa, njia hii si
nzuri kama njia nyingine zilizotajwa kuzuia mimba na kupanga uzazi.

Comments
Post a Comment